1Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake,
2Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,
3Lishangilieni jina lake takatifu,
4Mtafuteni Bwana na nguvu zake,
5Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,
6enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake,
7Yeye ndiye Bwana Mungu wetu,
8Hulikumbuka agano lake milele,
9agano alilolifanya na Abrahamu,
10Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,
11“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani
12Walipokuwa wachache kwa idadi,
13walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,
14Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;
15“Msiwaguse niliowatia mafuta;
16Akaiita njaa juu ya nchi
17naye akatuma mtu mbele yao,
18Walichubua miguu yake kwa minyororo,
19hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia,
20Mfalme alituma watu wakamfungua,
21Alimfanya mkuu wa nyumba yake,
22kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo
23Kisha Israeli akaingia Misri,
24Bwana aliwafanya watu wake kuzaana sana,
25ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake,
26Akamtuma Mose mtumishi wake,
27Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao,
28Alituma giza na nchi ikajaa giza,
29Aligeuza maji yao kuwa damu,
30Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia
31Alisema, yakaja makundi ya mainzi,
32Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe,
33akaharibu mizabibu yao na miti ya tini,
34Alisema, nzige wakaja,
35wakala kila jani katika nchi yao,
36Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao,
37Akawatoa Israeli katika nchi
38Misri ilifurahi walipoondoka,
39Alitandaza wingu kama kifuniko,
40Waliomba, naye akawaletea kware,
41Alipasua mwamba, maji yakabubujika,
42Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu,
43Aliwatoa watu wake kwa furaha,
44akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi
45alifanya haya ili wayashike mausia yake