1Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu;
2Ninawapa mafundisho ya maana,
3Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu,
4baba alinifundisha akisema,
5Pata hekima, pata ufahamu;
6Usimwache hekima naye atakuweka salama;
7Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima.
8Mstahi, naye atakukweza;
9Atakuvika shada la neema kichwani mwako
10Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia,
11Ninakuongoza katika njia ya hekima
12Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa;
13Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;
14Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu
15Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo;
16Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu;
17Wanakula mkate wa uovu,
18Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko,
19Lakini njia ya waovu ni kama giza nene;
20Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia;
21Usiruhusu yaondoke machoni pako,
22kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata
23Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo,
24Epusha kinywa chako na ukaidi;
25Macho yako na yatazame mbele,
26Sawazisha mapito ya miguu yako
27Usigeuke kulia wala kushoto;