1Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza
3Jikaze kama mwanaume;
4“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?
5Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake?
6Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini,
7wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,
8“Ni nani aliyeifungia bahari milango
9nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake,
10nilipoamuru mipaka yake,
11niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi;
12“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke,
13yapate kushika miisho ya dunia,
14Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri;
15Waovu huzuiliwa nuru yao,
16“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?
17Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti?
18Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia?
19“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi?
20Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake?
21Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa!
22“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji,
23ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu,
24Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa,
25Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi
26ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu,
27ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa,
28Je, mvua ina baba?
29Barafu inatoka tumbo la nani?
30wakati maji yawapo magumu kama jiwe,
31“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia?
32Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake,
33Je, unajua sheria zinazotawala mbingu?
34“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni,
35Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake?
36Ni nani aliyeujalia moyo hekima
37Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu?
38wakati mavumbi yawapo magumu,
39“Je, utamwindia simba jike mawindo,
40wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao,
41Ni nani ampaye kunguru chakula