We Believe JesusFé, Esperança e Nova Vida

Ayubu 39

Biblica® Toleo Wazi la Neno: Biblia Takatifu™ · suaíli

← Ayubu 38 Ayubu Ayubu 40 →

1“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa?

2Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo?

3Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao;

4Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani;

5“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru?

6Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake,

7Huzicheka ghasia za mji,

8Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho

9“Je, nyati atakubali kukutumikia?

10Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba?

11Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi?

12Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani

13“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha,

14Huyataga mayai yake juu ya ardhi,

15bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda,

16Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake;

17kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima,

18Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia,

19“Je, wewe humpa farasi nguvu

20Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige,

21Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake,

22Huicheka hofu, haogopi chochote,

23Podo hutoa sauti kando yake,

24Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi,

25Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’

26“Je, mwewe huruka kwa hekima yako

27Je, tai hupaa juu kwa amri yako

28Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku;

29Kutoka huko hutafuta chakula chake;

30Makinda yake hujilisha damu,

← Ayubu 38 Ayubu Ayubu 40 →