1Elihu akaendelea kusema:
2“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha
3Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali,
4Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo;
5“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu;
6Hawaachi waovu waendelee kuishi,
7Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki;
8Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo,
9huwaonyesha yale waliyoyatenda,
10Huwafanya wao kusikia maonyo,
11Kama wakitii na kumtumikia,
12Lakini wasiposikiliza,
13“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki;
14Wanakufa wangali vijana,
15Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao,
16“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki,
17Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu;
18Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri;
19Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi
20Usiutamani usiku uje,
21Jihadhari usigeukie uovu,
22“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake.
23Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake,
24Kumbuka kuzitukuza kazi zake,
25Wanadamu wote wameiona;
26Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu,
27“Yeye huvuta juu matone ya maji,
28mawingu huangusha chini maji yake,
29Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu,
30Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka,
31Hivi ndivyo atawalavyo mataifa,
32Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi,
33Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja;