1Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita,
3wakati taa yake iliniangazia kichwani changu,
4Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu,
5wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami,
6wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi,
7“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji
8vijana waliniona wakakaa kando,
9wakuu wakaacha kuzungumza
10wenye vyeo wakanyamazishwa,
11Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu,
12kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada,
13Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki,
14Niliivaa haki kama vazi langu;
15Nilikuwa macho ya kipofu
16Nilikuwa baba kwa mhitaji;
17Niliyavunja meno makali ya waovu,
18“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe,
19Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji,
20Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu,
21“Watu walinisikiliza kwa tumaini,
22Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi;
23Waliningojea kama manyunyu ya mvua
24Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha;
25Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao;