1Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema;
2Mafundisho yangu na yanyeshe kama mvua,
3Nitalitangaza jina la Bwana.
4Yeye ni Mwamba, kazi zake ni kamilifu,
5Wamefanya mambo ya upotovu mbele zake;
6Je, hii ndiyo njia ya kumlipa Bwana,
7Kumbuka siku za kale;
8Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao,
9Kwa kuwa fungu la Bwana ni watu wake,
10Katika nchi ya jangwa alimkuta,
11kama tai avurugaye kiota chake,
12Bwana peke yake alimwongoza;
13Akamfanya apande sehemu zilizoinuka za nchi,
14kwa jibini na maziwa kutoka makundi ya ngʼombe
15Yeshuruni32:15 Yeshuruni maana yake ni Yeye aliye mnyofu, yaani Israeli (ona pia Kum 33:26; Isa 44:2). alinenepa na kupiga teke;
16Wakamfanya Mungu kuwa na wivu kwa miungu yao migeni,
17Wakatoa dhabihu kwa pepo, ambao si Mungu:
18Mkamwacha Mwamba, aliyewazaa ninyi;
19Bwana akaona hili, akawakataa,
20Akasema, “Nitawaficha uso wangu,
21Wamenifanya niwe na wivu
22Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu,
23“Nitalundika majanga juu yao
24Nitatuma njaa kali dhidi yao maradhi mabaya,
25Barabarani upanga utawakosesha watoto;
26Nilisema ningewatawanya
27Lakini nilihofia dhihaka za adui,
28Wao ni taifa lisilo na akili,
29Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili,
30Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja,
31Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu,
32Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma,
33Mvinyo wao ni sumu ya nyoka,
34“Je, hili sikuliweka akiba
35Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.
36Bwana atawahukumu watu wake,
37Atasema: “Sasa iko wapi miungu yao,
38miungu wale waliokula mafuta ya dhabihu zao
39“Tazama basi, Mimi mwenyewe, Mimi Ndiye!
40Ninainua mkono wangu kuelekea mbinguni na kusema:
41wakati ninapounoa upanga wangu unaometameta
42Nitailevya mishale yangu kwa damu,
43Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,
44Mose na Yoshua32:44 Yoshua, yaani Yehoshea kwa Kiebrania, maana yake ni Yehova ni Mwokozi. mwana wa Nuni wakaja, wakanena maneno yote ya wimbo watu wakiwa wanasikia.
45Mose alipomaliza kuyasoma maneno haya yote kwa Israeli wote,
46akawaambia, “Yawekeni moyoni maneno yote ambayo nimewatangazia kwa makini siku hii ya leo, ili kwamba mpate kuwaagiza watoto wenu wayatii kwa bidii maneno yote ya sheria hii.
47Siyo maneno matupu tu kwenu, bali ni uzima wenu. Kwa hayo mtaishi maisha marefu katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
48Siku hiyo hiyo Bwana akamwambia Mose,
49“Kwea katika mapangano ya Mlima Abarimu hadi kilima cha Nebo kilichoko Moabu, ngʼambo ya Yeriko, na uitazame Kanaani, nchi ninayowapa Waisraeli kama milki yao wenyewe.
50Utafia kwenye mlima huo unaokwea na kukusanyika pamoja na watu wako, kama ndugu yako Aroni alivyofia juu ya Mlima Hori naye akakusanyika kwa watu wake.
51Hii ni kwa sababu ninyi wawili mlivunja uaminifu nami mbele ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba-Kadeshi katika Jangwa la Sini, na kwa sababu hamkuuinua utakatifu wangu miongoni mwa Waisraeli.
52Kwa hiyo, utaiona tu nchi kwa mbali; wewe hutaingia nchi ninayowapa watu wa Israeli.”