1Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia:
6kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10kutoka wana wa Yosefu:
11kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli:
21Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22Kutoka wazao wa Simeoni:
23Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24Kutoka wazao wa Gadi:
25Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26Kutoka wazao wa Yuda:
27Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28Kutoka wazao wa Isakari:
29Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30Kutoka wazao wa Zabuloni:
31Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32Kutoka wana wa Yosefu:
33Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34Kutoka wazao wa Manase:
35Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36Kutoka wazao wa Benyamini:
37Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38Kutoka wazao wa Dani:
39Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40Kutoka wazao wa Asheri:
41Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42Kutoka wazao wa Naftali:
43Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.