We Believe JesusFé, Esperança e Nova Vida

Yoshua 12

Biblica® Toleo Wazi la Neno: Biblia Takatifu™ · suaíli

← Yoshua 11 Yoshua Yoshua 13 →

1Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:

2Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.

3Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi12:3 Yaani Bahari ya Galilaya. hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi12:3 Yaani Bahari Mfu.), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.

4Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.

5Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.

6Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.

7Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:

8nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):

9mfalme wa Yeriko

10mfalme wa Yerusalemu

11mfalme wa Yarmuthi

12mfalme wa Egloni

13mfalme wa Debiri

14mfalme wa Horma

15mfalme wa Libna

16mfalme wa Makeda

17mfalme wa Tapua

18mfalme wa Afeki

19mfalme wa Madoni

20mfalme wa Shimron-Meroni

21mfalme wa Taanaki

22mfalme wa Kedeshi

23mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) 12:23 Au: katika miinuko ya Nafoth-Dori.

24mfalme wa Tirsa

← Yoshua 11 Yoshua Yoshua 13 →