1Kisha Elihu akasema:
2“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima;
3Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno
4Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa,
5“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia,
6Ingawa niko sawa,
7Ni mtu gani aliye kama Ayubu,
8Ashirikianaye na watenda mabaya
9Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote
10“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu.
11Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda;
12Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa,
13Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia?
14Kama lilikuwa kusudi la Mungu,
15wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja,
16“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili;
17Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala?
18Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’
19yeye asiyependelea wakuu,
20Wanakufa ghafula, usiku wa manane;
21“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu;
22Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa,
23Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana,
24Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi
25Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote,
26Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao
27kwa sababu wameacha kumfuata Mungu,
28Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake,
29Lakini kama akinyamaza kimya,
30ili kumzuia mtu mwovu kutawala,
31“Kama mwanadamu akimwambia Mungu,
32Nifundishe nisichoweza kuona;
33Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako,
34“Wanadamu wenye ufahamu husema,
35‘Ayubu huongea bila maarifa;
36Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho,
37Kwenye dhambi yake huongeza uasi;